Mapishi







 

Wednesday, 5 October 2011

Seabass wa kuokwa na chips (takeaway)



Hii pia ni moja ya favorite takeaway yangu. Mara nyingi huwaga nikichoka kula vyakula vya kichinese na vya kihindi au nandos huwa napenda kula samaki wa kuokwa katika mgahawa wa kilebanese ninaoupenda. Hapa nili-order samaki wa kuokwa na chips na salad. Huu ni mlo mzuri wa afya isipokuwa chips tu. Kama ukitaka kuoka samaki mzima kama huyu, muhimu tu kumkata miraba kila upande na kum-marinate masaa matatu hadi sita ili aingie viuungo vizuri na kumuoka kila upande dakika kumi katika moto usiokuwa mkali sana.

Wednesday, 28 September 2011

Mapishi ya samaki aina ya salmon


Wakati mwingine mtu unakuwa umechoka na usingependa kupoteza muda jikoni, so mlo wa chapchap unakuwa ni wazo zuri, Mlo huu ni rahisi kuuanda na hata haikuchukui zaidi ya dakika ishirini chakula kinakuwa tayari mezani.

Mahitaji
Salmon fillet 2
Potatao wedge kiasi
Lettice kiasi
Cherry tomato
Limao 1
Swaum
Chumvi
Olive oil

Matayarisho
Mmarinate samaki na chumvi, swaum na nusu ya limao kisha muweke pembeni, baada ya hapo washa oven kisha tia potato wedge zikisha karibia kuiva anza kumpika samaki, tia mafuta kidogo sana kama kijiko kimoja cha chai hivi katika frypan isiyoshika chini yakisha pata moto kiasi muweke samaki wako (upande wenye ngozi chini kwanza) Mpike mpaka uone rangi ya kahawia kwa chini kisha mgeuze upande wa pili, uku samaki wako akiwa anaendelea kuiva, tayarisha salad yako kwa kusafisha lettice na nyanya kisha zichanganye pamoja kisha tengeneza salad dressing pembeni , kamua limao kisha tia olive oil na chumvi kidogo, Baada ya hapo samaki na potato wedge vitakuwa vimeiva, andaa mlo wako na utakuwa tayari kwa kuliwa.

Thursday, 22 September 2011

Mapishi ya mboga mchanganyiko


Mahitaji
Viazi ulaya 4 vya wastani
Hoho jekundu 1/2
Hoho la njano 1/2
Hoho la kiajani 1/2
Njegere 1 kikombe cha chai
Carrot 1 kubwa
Broccoli kidogo
Cauliflower kidogo
Kitunguu 1
Nyanya 1/2 kopo
Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chakula
Curry power 1 kijiko cha chakula
Coriander powder 1 kijiko cha chai
Tarmaric 1/2 kijiko cha chai
Olive oil
Chumvi
1/4 ya limao

Matayarisho
Katika sufuria isiyoshika chini kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia swaum/tangawizi na spice zote kaanga kwa muda mfupi kisha tia nyanya na chumvi. pika mpaka nyanya ziive kisha tia vegetable zote na vimaji kidogo sana na kisha kamulia limao, baada ya hapo punguza moto na kisha funika na zipike mpaka vegetable zote ziive na rojo ibakie kidogo. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.

Friday, 16 September 2011

Mapishi ya choroko


Mahitaji
Choroko kikombe 1 na nusu
Nazi kopo 1
Kitunguu kikubwa 1
Nyanya 1/2 kopo
Swaum 1 kijiko cha chai
Curry powder 1 kijiko cha chai
Chumvi kiasi
Olive oil
Pilipili nzima

Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima kisha zichemshe mpaka ziive na ziweke pembeni. Baada ya hapo saga pamoja nyanya, kitunguu, na swaum kisha vipike mpaka maji yote, baada ya hapo tia mafuta na curry powder, pika mpaka nyanya zitoe mafuta kisha tia choroko,tui la nazi, maji nusu kikombe,pilipili na chumvi, kisha koroga vizuri na uache ichemke. Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na rojo ibakie kidogo sana, kisha ipua na mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Mi huwa napenda kuila na wali ila hata na ugali au chapati inaenda pia.

Monday, 12 September 2011

Jinsi ya kutengeneza coleslaw


Mahitaji
Kabichi iliyokatwa nyembamba 2 vikombe
Carrot iliyokwaguliwa 1
Kitunguu 1/4 kilichokatwa vyembamba
Yogurt au mayonnise 1/2 kikombe
Limao 1/4
Chumvi kiasi

Matayarisho
Katika bakuli safi changanya vitu vyote mpaka mchanganyiko wako uchanganyike vizuri, kisha iweke frijini kwa muda mchache ili chumvi na limao viingie katika kabichi na carrot. Baada ya hapo caleslaw yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Hii ni moja wapo aina ya salad na mara nyingi pindi watengenezapo hupenda kutumia mayonnise, Ila kwa mimi hupenda kutumia yogurt badala ya mayonnise.kwa maana mayonnise ina mafuta sana. Kwa hiyo hapo chaguo ni lako unaweza tumia mayonnise au yogurt.Unaweza kulia na chips,nyama au chochote upendacho.

Wednesday, 7 September 2011

My favorite takeaway

Saturday, 3 September 2011

Mapishi ya Kabichi


Mahitaji
Kabichi  1/2 kilo
Nyanya ya kopo 1/2
Kitunguu 1
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Chumvi
Olive oil

Matayarisho
Kwanza kabisa bandua magada ya juu ya kabichi, kisha ioshe na uikaushe maji baaba ya hapo katakata kabichi (inapendeza zaidi kama ikikatwa nyembamba) kisha saga pamoja nyanya na kitunguu. Baada yahapo tia katika sufuria ya kupikia, ipike mpaka maji yote yatakapokauka kisha tia chumvi, curry powder na mafuta pika kwa muda kiasi kisha tia kabichi na upunguze moto. Pika mpaka kabishi itakapoiva kisha ipua na itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuila kwa wali au ugali.

2 comments:

  1. Default Jinsi ya kujipikia maandazi

    Mandazi

    Mandazi (or Maandazi, also called Mahamri or Mamri) are East African fried breads similar to doughnuts (donuts) popular in the coastal Swahili areas of Kenya and Tanzania and popular "upcountry". They are eaten with tea or coffee for breakfast, for a snack anytime, and with the main course for lunch or dinner. They are not as sweet as U.S. style doughnuts and do not have a sugar glaze or icing.
    main street, zanzibar

    What you need

    * two cups warm water
    * two teaspoons baking powder -- or -- one teaspoon dry yeast
    * four cups all-purpose flour
    * one-half cup sugar
    * one-quarter teaspoon spice (one or more of the following to total one-quarter teaspoon: cardamom, cinnamon, allspice, ginger)
    * two tablespoons butter, margarine, or vegetable oil
    * one-quarter cup warm milk (optional)
    * one egg, lightly beaten (optional)
    * pinch of salt
    * oil for deep frying

    What you do

    * All pastry ingredients should be allowed to come to room temperature if they have been in the refrigerator. If using yeast: mix the yeast with a few spoonfuls of the warm water.
    * In a mixing bowl combine the flour, baking powder (if not using yeast), sugar, and spice (cardamom is most common in Eastern Africa). Add the yeast. Mix the water, butter (or margarine, or oil), milk, and egg together. Gradually add this mixture to the flour while kneading into dough. (If not using milk and egg use additional water as necessary.) Knead until a smooth and elastic dough is formed -- fifteen to twenty minutes. If using yeast: Place dough in a clean bowl, cover with a cloth, and allow to rise in a warm place (such as on oven that has been heated to 100 degrees Farenheit then turned off) for an hour or more. If using baking powder, let dough rest for several minutes.
    * Divide the dough into several hand-sized pieces. Roll or press the pieces into circles about one-half inch thick. Cut circles into halves or quarters (or whatever you like). Some cooks (when using yeast) place the doughs on a cookie sheet and let them rise a second time.
    * Heat a few cups of vegetable oil to 300 degrees Farenheit in a skillet or deep pot. Fry the doughs in the hot oil, turning a few times, until they are golden brown all over. Fry only as many together as can float in the oil without touching one another. Place on paper towels to drain. Serve warm.

    ReplyDelete
  2. Nyumbani
    Sambusa Za Nyama

    Vitafunio

    VIPIMO

    Manda ya sambusa ya tayari Kiasi zinavyouzwa

    (Kiasi ya sambusa 40-50)

    Mafuta ya kukaangia Kiasi

    Nyama ya Kusaga 3LB (Pounds)

    Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 Vijiko vha chai

    Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai

    Pilipili manga 1 kijiko cha supu

    Garam masala 1 kijiko cha supu

    Chumvi Kiasi

    Vitunguu maji vilivyokatwa

    (chopped) 3 Vidogo au 2 Vikubwa

    Kotmiri iliyokatwa (chopped) Kiasi



    NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA



    1. Pika nyama ya kusagwa kwa kutia chumvi, thomu na tangawizi, pilipili na ndimu.

    2. Kabla haija kauka tia Garam masala.

    3. Zima moto acha kidogo ipoe tia vitunguu na kotimiri.

    4. Funga sambusa katika manda kama kawaida.

    5. Pika sambusa katika mafuta ya moto hadi ziwe nyekundu na zikiwa tayari kuliwa.

    ReplyDelete